Posts

Showing posts from August, 2022

KUJAA MAJI KWENYEGOTI/KNEEL EFFUSION.

Image
Maji Kwenye Goti Ni Tatizo Gani? Maji kwenye goti (knee effusion au water on the knee) ni hali ya kupata maumivu makali kutokana na maji kujaa kuzunguka au ndani ya maungio ya mifupa ya kwenye goti (knee joint). Hali hii ikitokea, kujua chanzo na dalili zake na njia bora ya kuyaondoa maji hayo kwenye goti ni kitu muhimu. Njia utakayoitumia kuuondoa uvimbe huu itategemea chanzo cha uvimbe na daktari anaweza kuhitajika kufanya uchunguzi. Kiasi kidogo cha maji huwepo kwenye joint ya kawaida. Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 27 ya watu hupata tatizo la maji kwenye magoti kwa muda fulani. Umbile  La Goti   Goti ni jointi iliyo kubwa na yenye sehemu nyingi kuliko jointi zote katika mwili. Jointi ya goti huunganisha mfupa wa paja (femur) na mfupa wa chini ya goti (tibia). Mfupa mdogo unaokwenda sambamba na mfupa wa chini ya goti (fibula) na kifuu cha goti (patella) ni mifupa mingine inayojenga jointi ya goti. Tendoni huiunganisha mifupa ya goti na misuli ya miguu amba

VYAKULA VYA KUEPUKA UKIWA NA GOUT

Image
Chakula Cha Kukwepa Ukiwa Na Gout   Gout ni ugonjwa unaosababisha maumivu makali ya maungio ya mifuapa (joints). Gout huleta hushambulia joint moja au zaidi, lakini mara nyigni hutokea miguuni. Mashambulizi hutokea wakati uric acid inapoganda na kujijenga kwenye joints. Uric acid, ambayo ni antioxidant inayolinda utando wa ndani wa mishipa ya damu, huzalishwa mwilini wakati chakula cha kundi la purines kikivunjwavunjwa. Kupata au kutopata gout kunategemea zaidi urithi.  Mabadiliko katika namna ya kuishi yanaweza kuzuia maumivu. Kuwa mwangalifu na vitu unavyokula na kuacha kula chakula chenye purines kwa wingi kunaweza kukuondolea dalili za gout.   Nyama Zinazoleta Gout Nyama za viungo zinatakiwa kuachwa kabisa kama una  ugonjwa wa gout  kwa sababu zina viwango vikubwa vya purines. Nyama hizo za viungo ni kama: maini, kongosho za ndama au kondoo, figo, ubongo, na utumbo unaoliwa. Nyama nyingine zote zinatakiwa kuliwa kwa kiasi, kiasi kisichozidi wakia (ounce) 4, sasawa na uk

UGONJWA WA GOUT/GAUT DISEASE

Image
Nini Chanzo Na Tiba Yake? Gout ni ugonjwa ambao umefahamika kwa miaka mingi sana. Inasadikika kuwa watu wa kwanza kuutambua ugonjwa huu walikuwa watu wa Misri, kunako miaka ya 2640BC. Mtaalamu wao wa tiba Hippocrates aliuita ugonjwa huu “Ugonjwa Wa Kumfanya Mtu Asitembee” na aliuhusisha ugonjwa huu na namna ya mtu anavyoishi. Hadi hivi leo ugonjwa huu ni tatizo la jamii nyingi, ambao huwapa maumivu makali sana wale ambao wameathirika. Kwa bahati nzuri ugonjwa huu hutibika na kuna hatua za kuchukua zinazoeleweka ili usipatwe na ugonjwa huu. Katika ukurasa huu tutatazama ugonjwa wa gout ni nini , chanzo cha ugonjwa wa gout, dalili zake na namna ya kuutibu pale unapokuwa umeathirika.  Gout Ni Nini? Gout ni namna moja ya Arthritis, ugonjwa ambao hushambulia joints (sehemu za maungio ya mifupa). Huu ndiyo ugonjwa wa joints ambao huwashambulia sana na kuwapa maumivu makali wanaume. Wanawake pia huweza kuathirika na ugonjwa huu hasa baada ya kukoma hedhi. Ugonjwa huu huleta maumiv