𝗧𝗘𝗭𝗜𝗗𝗨𝗠𝗘 𝗡𝗜𝗡𝗜𝗡𝗜?

𝗧𝘂𝗷𝗶𝗳𝘂𝗻𝘇𝗲 𝗷𝘂𝘂 𝘆𝗮 𝘁𝗲𝘇𝗶𝗱𝘂𝗺𝗲 (Benign prostatic hyperplasia BPH)

Kila mwanaume anazaliwa na Tezi ya kiume. Tezi dume siyo ugonjwa bali ni kiungo kama viungo vingine mwilini. Tezi dume inapatikana katika mfumo wa uzazi wa mwanaume katika shingo ya kibofu cha mkojo. Kazi yake kubwa nikutengeneza majimaji ya uzazi wa mwanaume (shahawa), ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizo tengenezwa kutoka kwenye Korodani; na husaidia mbegu za kiume kubaki hai kwa muda unaostahili pia kumkinga mwanaume na maambukizi katika mfumo wa mkojo.

Tatizo linakuja kiungo hiki kinapoanza kutanuka. Kiungo hiki kinatanuka taratibu taratibu mnoo. Hili ni tatizo linalo wakumba wanaume wengi.

Takwimu zinaonesha kwamba kati ya wanaume 10, wa 5 na kuendelea wana dalili za kutanuka kwa Tezi dume.

UKUAJI WA TEZI DUME.

Ukuwaji wa Tezi dume ni ile hali ya chembe chembe hai katika tezi ya kiume kukua bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili katika eneo linalo zunguka mirija ya kupitisha mkojo na mbegu za kiume.
 Tatizo hili kwa sasa linawapata wanaume kuanzia umri wa miaka 25 na kuendelea, tofauti na awali lilikuwa miaka zaidi ya 50.
Takwimu kutoka kwenye shirika la CHRP (Centre for Human Right Promotion), zinaonesha kwamba kiujumla kila mwanaume katika maisha yake ana 16% za kugundulika na saratani ya Tezi Dume, mtu 1 kati ya watu 6 analo hili tatizo; Na 3% (1 kati 33) wanakufa kwasababu ya Saratani ya Tezi Dume.
 Saratani hii inaua mwanaume mmoja kila baada ya dakika 13.

II. VYANZO VINAVYOPELEKEA TEZI DUME KUTANUKA

Tatizo la kutanuka kwa tezi dume limekuwa kwa kasi sana hii ni kutokana na mitindo ya maisha wanaume wengi wanayoishi. Pia na elimu ndogo iliyoko kwenye jami kuhusu afya bora na  Virutubisho.

Vifuatavyo ni vyanzo vya kutanuka kwa tezi dume:
- Ukosefu wa lishe kamili na upungufu wa Virutubisho muhimu mwilini
- Uwepo wa sumu nyingi na mafuta mengi mwilini hasa katika mishipa na ogani za uzazi
- Kutokufanya mazoezi
- Matumizi ya pombe kali, na uvutaji wa sigara
- Uzito mkubwa (uliopindukia, uliokithiri), na Kitambi
- Kutokukaa sawa kwa vichocheo vya mwili (Hormone Imbalance)
-       Msongo wa mawazo (Stress )
-       Magonjwa ya zinaa
- Umri mkubwa
- Upasuwaji wa korodani,matatizo ya kimaumbile ya Korodani
-       Historia ya Familia (Kurithi)
-       Mazingira (Ethnicity)n.k

III. DALILI ZA KUTANUKA KWA TEZI DUME

Tatizo la Tezi Dume si tatizo la kutokea tuu siku moja na mara moja tuu na ndo maana tunasisitiza sana matumizi ya Suppliments (Virutubisho)  kwa mwanaume yeyote anaejari Afya yake. Mpaka mtu apate saratani ya Tezi Dume (Prostate Cancer), atambue alianza kupata tatizo hilo kwa muda mrefu sana, Wengi wao hueleza dalili za tatizo hili huanza kuziona si chini ya miaka  3.
Hii hutokana na mrundikano wa mkojo unaobaki kwenye kibofu na kwenye mrija wa mkojo (Urethra) wakati unakojoa, ukiendelea kujirundika kwenye kibofu na mrija; baada ya muda unazalisha “Uric Acid” na ndio inatengeneza saratani (cancer).

Saratani ziko stage nne.
 Ya kwanza na yapili ukiwahi unaweza kupona; lakini ikishafika stage ya 3 na 4, hazitibiki. Unasaidiwa kupunguza makali kwa mionzi ukijitayarisha kupoteza maisha muda wowote.

Hivyo ukiona dalili mojawapo kati ya hizi chukua tahadhari na hatua mapema kabla hujaharibu mfumo wako
mzima wa uzazi wa mwanaume.

a) Dalili za awali

- Kukojoa mkojo uliochanganyikana na damu
- Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
- Maumivu kwenye mfumo wa mkojo
- Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
- Kuhisi kibofu kimeja mkojo muda wote na ukienda kukojoa mkojo hautoki, lakini ukirudi kukaa unahisi kukojoa tena.
-       Homa
- Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
- kupata maumivu ukilazimisha kukojoa na kushindwa kutoa mkojo pale unapolazimisha na kuambatana na maumivu makali.

b) Dalili za mtu aliyeathirika

- Maumivu ya mifupa hasa chini ya mgongo, kiuno na mbavu
-       Miguu kuwa dhaifu
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa, au Kuhisi maumivu makali wakati unamaliza tendo la ndoa
- Kushindwa kuzuia mkojo , pindi unapohisi kukojoa
- Kushindwa kuzuia haja kubwa
(kinyesi cha maji maji)
- Tumbo kujaa gesi mara kwa mara

IV. MADHARA YA TEZI ILIYOTANUKA

Katika hatua za awali, tezi inapotanuka hugunduliwa kwa kupimwa kwa njia ya kidole.

Hii ni njia ambayo daktari huingiza kidole kwenye njia ya haja kubwa ili kuweza kubaini kama tezi imetanuka. Kipimo hiki ndicho rahisi kinacho kubalika duniani kote na kisicho na gharama. Lakini kimekuwa kikipata upinzani kutoka kwa wanaume kutokana na imani potofu ya wahusika wa tatizo hili kuona ni udhalilishaji.
Kipimo kingine ni kipimo cha damu. Damu huchunguzwa aina ya protein inayozailishwa na seli za tezi dume, kiitwacho Prostate Antigen (PSA). PSA huonesha kuwapo kwa tatizo kwenye Tezi Dume, lakini kipimo hiki hakina uwezo wa kutofautisha endapo tatizo hilo linamaanisha saratani.

MADHARA:
Yafuatayo ni madhara ya tezi iliyotanuka:
- Kibofu cha mkojo kuuma : hivyo hupelekea mkojo kurudi juu, na kuharibu figo na Ini n.k.
- Kufunga kwa njia ya mkojo kabisa
- Figo kushindwa kufanya kazi (Kidney Failure)
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa (Ndoa zinavunjika)
- Ugumba (Infertility, Frigidity for men)
- Kutokea kwa majipu sehemu ya Tezi Dume
-       Kifo

V. SULUHISHO KWA TEZI ILIYOTANUKA

a) Suluhisho Linalopendwa na 
Watu wengi  pindi wanapopatwa na madhara ya Tezi dume ni Dawa na kujikuta wakipewa tiba ambazo huficha tatizo hilo kwa muda mfupi kisha tatizo hujirudia kwa kasi kubwa.
Tezi iliyotanuka haiwezi kutibika kwa njia za madawa yenye makemikali au mitishamba, lakini madawa au upasuaji hupunguza maumivu ya dalili na kuzifanya zisizidi sana.
Kuna njia 3 za kudhibiti Tezi iliyotanuka
1. Kusubiri na kufuatilia kwa ukaribu na Daktari:
Inashauriwa kwamba kwa tatizo hili ni bora kuendelea kulichunguza bila kukimbilia tiba kali kama madawa, upasuaji na Tiba kemikali, mpaka pale mtu atakapoona hakuna njia mbadala.
2. Madawa
“Baadhi ya madawa wanayopewa wagonjwa wa saratani ya tezi Dume yaligunduliwa miaka 30 iliyopita, yanasababisha athari kwenye Ini, Moyo na kuvimbisha magoti. Yamepigwa marufuku katika Nchi haswa za Ulaya.”
– Johnathon Waxman , Cancer Specialist, Hammer Smith Hospital, London
3. Upasuaji
Njia hii ambayo madaktari hutumia inapelekea “70% ya wagonjwa kuwa mahanithi baada ya upasuaji, na 40% wanashindwa kuzuia mkojo kutoka wanapo banwa na haja ndogo.”
– Johnathon Waxman
Inasikitisha kuona wanaume wanapasuliwa bila uhakika wowote kwamba huo upasuaji utakuwa na manufaa.

b) Suluhisho la kudumu (Bora)

JE NINI WAWEZA KUFANYA  KUJIKINGA NA KUONDOKANA NA CHANGAMOTO YA TEZI DUME??.

SOMA HAPA:
Miili yetu hihitaji virutubisho muhimu ili kuimarisha Kinga na Kuulisha mwili wetu.

Vitu gani vya kuzingatia kuilinda tezi dume?

1. Kula mboga mboga na matunda kwa wingi kulingana na kundi lako la damu yako.
2. Punguza au acha kuvuta sigara
3. Punguza au acha utumiaji wa pombe kali.
4. Punguza kukaa kwa mda mrefu sehemu moja kwa siku.
Fanya mazoezi kwa wingi.(Sitting is a new smoking)
5. Kutovaa nguo za kubana
6. Vaa chupi za cotton na sio material yeyote.
7. Kuhakikisha Uume uwe una erect mara kwa mara
8. Na mwisho Zingatia Matumizi ya Virutubisho. Utumiaji wa virutubisho ( Supplements) hasa vinavyohusika na Tezi dume, Uzazi kwa mwanaume(Nguvu za kiume) pamoja na ogani zote za uzazi.

Tezi Dume inatanuka kwasababu ya upungufu wa madini na virutubisho mwili unavyohitaji.
Kwa watu wenye uhitaji wa kujikinga na pia wenye changamoto hii ya kutanuka kwa Tezi Dume, na mfumo wa uzazi mwanaume ,na 
Kampuni tumewaandalia program ya lishe kamili na virutubisho muhimu . Supplements hizi ni vyakula, siyo madawa wala mitishamba. Zimetengenezwa kutoka kwenye vyakula ambavyo tungefaa kula kila siku, na vina lishe kamili na virutubisho muhimu katika miili yetu inavyo hitaji ili iweze kutengeneza mfumo bora wa mwili na uzazi wenye afya bora na nadhifu.

Supplements hizi (Virutubisho) vina  mchanganyiko wa  Proteins, Vitamins, Minerals, Essential Fat Acid and Trace minerals .
Pia Program zetu za lishe zimethibitishwa na mashirika ya kuthibiti ubora wa viwango vya bidhaa duniani. Na kwa hapa Tanzania, zimethibitshwa na mamlaka ya chakula na madawa (TMDA) pamoja na (Tbs) viwango vya ubora Tanzani

@𝐃𝐫_𝐄𝐯𝐢𝐭𝐮𝐬

Comments

Popular posts from this blog

What are Kidney Stones?